Tottenham Hotspur, Chelsea na Arsenal zinadaiwa kupanga kumsajili mshambuliaji wa Manchester United, Marcus Rashford (28). Hata hivyo, viongozi wa Manchester United hawataki kumuuza kwa klabu nyingine ya Ligi Kuu ya England.
Mlinda lango wa Aston Villa na timu ya taifa ya Argentina, Emiliano Martínez (33), anawindwa na Juventus, huku Arsenal ikimfuatilia beki wa Aston Villa na England, Ezri Konsa (28).
Nottingham Forest ipo katika mazungumzo ya hatua za mwisho kumsajili beki wa Sporting CP na Ivory Coast, Ousmane Diomande (22).
Beki wa kati wa West Ham United, Jean-Clair Todibo (26), anahusishwa na uhamisho kwenda Juventus.
Manchester United bado inatafuta kiungo wa kati, lakini imepunguza nia ya kuwasajili Carlos Baleba (22) wa Brighton na Alex Scott (22) wa Bournemouth kutokana na gharama kubwa za usajili wao.
Bournemouth imeazimia kumbakisha Alex Scott licha ya mchezaji huyo wa timu ya vijana ya England chini ya miaka 21 kukataa kusaini mkataba mpya. Arsenal inaendelea kumfuatilia.
Ipswich Town imefikia makubaliano ya awali kumsajili mshambuliaji wa Celtic na Japan, Daizen Maeda (28), kwa ada ya pauni milioni 8 pamoja na nyongeza ya pauni milioni 2 kulingana na mafanikio.
Beki wa kulia wa Manchester United, James Overy (18), raia wa Australia, anafuatiliwa na Rangers pamoja na klabu kadhaa kutoka Australia.
Facts Only
* Tottenham Hotspur, Chelsea, and Arsenal are reportedly negotiating the transfer of Marcus Rashford from Manchester United.
* Manchester United leadership does not wish to sell Marcus Rashford to another English Premier League club.
* Juventus is pursuing Emiliano Martínez from Aston Villa.
* Arsenal is following Ezri Konsa from Aston Villa.
* Nottingham Forest is in final negotiations regarding Ousmane Diomande from Sporting CP and Ivory Coast.
* Jean-Clair Todibo from West Ham United is linked to a transfer to Juventus.
* Manchester United is seeking a midfielder but has reduced interest in signing Carlos Baleba from Brighton and Alex Scott from Bournemouth due to high transfer fees.
* Bournemouth intends to keep Alex Scott despite being under 21.
* Ipswich Town reached preliminary agreements to sign Daizen Maeda from Celtic and Japan for eight million pounds plus two million based on performance.
* James Overy from Manchester United is followed by Rangers and several Australian clubs.
Executive Summary
Full Take
Sentinel — Human
The text functions as a collection of fragmented football transfer rumors. It exhibits characteristics of journalistic summary rather than synthetic generation, focusing on reporting reported speculation.
