Ushahidi waendelea kutolewa mahakamani
Jaji: shahidi kiapo chako kinaendelea naamini unakumbuka ulipoishia
Wakili: Baada ya kupata taarifa kwa ma RCO wa mikoa mbalimbali nini kiliendelea
Shahidi: Hatua iliyofuata niliitisha majalada nikiwa na lengo la kusoma na kufahamu ushahidi uliopo ndani ya hayo majalada
Wakili: ni mikoa ipi na ipi?
Shahidi: Mfano mkoa wa kilimanjaro lenye KR/CIB/PE/18/2025 hili lilikuwa jalada la uchunguzi toka Kilimanjaro, Arusha Ars/CIB/PE/40/2025, Mbeya MBE/CID/PE/54/2025 pia kuna jalada lilitoka Ruvuma likiwa na kumbukumbu namba …. ambalo lilikuwa na kosa la kula njama za kuandamana
Pia kulikuwa na jalada toka mkuu wa upelelezi Kinyerezi
Wakili: Baada ya kuitisha haya majalada unakumbuka nini?
Shahidi: Baada ya kuyapokea niliyasoma
Wakili: Baada ya kuyasoma yalikuwa kwenye hatua gani za upelelezi Shahidi: Baada ya kuyasoma tulibaini wengi waliokuwa kule walikuwa wamehamasika na kauli ya mshitakiwa na tukabaini wengi wao walikuwa wafuasi wa Chadema na wengine wachache wa vyama vingine
Wakili: Baada ya kugundua wengi wao walikua ni wafuasi kilifuata nini?
Shahidi: Nilielekeza majalada yarudi mikoani na nikaelekeza hawa watu watafutwe na waandikwe maelezo kama mashahidi.
Wakili: Waandikwe maelezo kama mashahidi kwenye kesi gani?
Shahidi: Kwenye kesi hii tuliyonayo ya uhaini jambo ambalo liletelekezwa wahusika walipatikana na wakaandikishwa maelezo
Wakili: Baada ya kupata hayo maelezo hasa wewe ulifanya nini?
Shahidi hayo maelezo yaliwekwa kama sehemu ya jalada la ushahidi dhidi ya mtuhumiwa.
Wakili: Unakumbuka nini juu ya tarehe 9/4/2025
Shahidi: Hii ndio tarehe aliyokamatwa mshitakiwa akiwa ziarani mbinga wakili alafu baada ya kukamatwa
Shahidi: Alisafirishwa siku hiyo hiyo na kuletwa Dar es salaam na alifika kesho yake tarehe 10/04/2025 na kufikishwa kituo cha kati cha polisi alifikishwa na kusomewa tuhuma zake na mtuhumiwa alisema hakua tayari kutoa maelezo pale na alisema atatolea maelezo yake mahakamani.
Wakili: Kisha nini kikaendelea? Shahidi: Baada ya kupata maelezo yako ofisi ya taifa ya mashtaka ya kanda ya DSM ilipofika majira ya mchana iliandaa mashitaka dhidi ya mshitakiwa na jioni ya hiyohiyo siku alifikishwa mahakama ya hakimu mkazi kisutu.
Wakili: Nini kikafuata?
Shahidi: Nakumbuka baada ya kusomewa mashitaka Jalada la upelelezi lilirejeshwa kwetu kwa ajili ya upelelezi zaidi.
Wakili: Nini unakumbuka kingine?
Shahidi:Tukiwa tunaendelea na upelelezi tulipokea malalamiko toka kwa baadhi ya mashahidi kuwa kuna matishio kwao iwapo wangetoa ushahidi dhidi ya mshitakiwa.
Wakili: Hao waliokua wanatoa vitisho mlibaini ni nani?
Shahidi: Wengi walikuwa ni wafuasi wa chadema tena wakitumia maneno ya kuwasalimia na kwenda mbali ya kusema waombewe mabaya wapate mikosi na laana.#
Wakili: Baada ya kupokea hiyo taarifa mlifanya nayo nini?
Shahidi: Na sisi kwa nafasi zetu tuliingia kwenye mitandao na comments zenyewe zilikuwa na vitisho kwenye mitandao ya facebook, tiktok instagram na x
Wakili: Baada ya kujiridhisha...?
Shahidi: Baada ya kujiridhisha nilifanya mawasiliano na ofisi ya taifa ya mashitaka kueleza juu ya matishio hayo kwa mashahidi ili kuomba wafichwe (ulinzi)
Wakili: Nini kikafuata?
Shahidi: Baada ya hapo nilikwenda kuchukua kiapo maalumu toka ofisi ya taifa ya mashitaka ili mashahidi hao wapatiwe ulinzi
Wakili: Mheshimiwa jaji baada ya kuwauliza wenzangu hakuna swali la nyongeza.
Unaweza kusoma;
